KARIBUNI SA

Thursday, December 30, 2010

BOBBY FARREL WA BON M AFARIKI DUNIA


Boby Farrell wa BON M wakati wa uhai wake

Boby Farrell wa BON M afariki dunia mjini St.Petersburg,Urusi

Boby Farrell (61) alikuwa mwanamuziki mashuhuri katika miaka 1970 kutoka kundi maarufu enzi hizo linalofahamika kama Boney M,Mr. Boby Farrell amekutwa amefariki katika chumba cha hoteli alichofikia huko mjini St.Petersburg, Urusi.

Mwanamuziki huyo alikuwa katika ziara ya kimziki nchini Urusi, maiti yake iligunduliwa katika chumba alichofikia baada ya kumaliza show zake.idara ya usalama ya St.Peterburg imeunda kamati maalum ya kuchunguza kifo cha Bobby Farrell.

Marehemu Bobby Farrell alikuwa mwanamuziki anayeongoza safu ya mbele iliyokuwa bendi maarufu duniani Boney M, ambapo alifanya kazi na mwanamuziki Maisie Williams, Liz Mitchel na Marcia Barret.

Kundi la Bon M lilijizolea umarufu kila kona duniani kutokana na umahiri wa nyimbo zake kutingisha katika madisco na redio za kimataifa. Kundi hili lilikuwa na maskani yake nchini Ujerumani na kuweza kupiga tour kila kona duniani.

Baada ya kundi la Bon M kusambaratika marehemu Bobby Farrell alihamishia makazi yake mjini Amsterdam, Uholanzi.

Bobby Farrell ambaye ametamba na nyimbo zake akiwa na Boney M ambazo hupendwa sana kipindi hiki cha kusherekea Christmas na mwaka mpya hatunae tena duniani. Bobby Farrell ni moja ya wanamuziki watanashati sana duniani.

Thursday, December 23, 2010

MGOMO WA WANAFUNZI UDOM – CSSH

Jumapili ya tarehe 18/12/2010 usiku kumkia jumatatu wanachuo wa skuli ya sayansi ya jamii na sayansi ya lugha walianza mgomo wa kuishinikiza serikali juu ya matatizo yanayowakabili. Moja ya matatizo yaliyoanishwa na bunge la serikali ya wanafunzi ambalo lilibariki na kupitisha mgomo huu ni kutokuwepo kwa mafunzo ya vitendo kwa baadhi ya kozi zipatazo kumi na nne katika skuli hii.Madai ya wanafunzi hawa yamekuwa hayasikilizwi na kusababisha waamue kuandamana hadi kwa waziri mkuu mheshimiwa Mizengo Pinda.

Kulia mwenye koti la kijani ni Leonard Singo ambaye ni Rais wa skuli ya sayansi ya jamii na sanaa ya lugha (CSSH) akiongea na mkuu wa mkoa wa Dodoma Mh. Msekela baada ya maandamano kuzuiwa na askari polisi kwenye lango la kuingia chuoni na katikati ni Mkuu wa skuli hii Pro. Casmir Rubagumya


Hapa ni mlezi au dean of student Mr.Manongi akiteta jambo


Askari wa kutuliza ghasia FFU wakiwa tayari kusubiri amri ya kutoa kichapo siku hiyo

wanachuo wakiwa tayari kwa lolote na wengi wao wakiwa wamebeba maji kwa ajili ya kunawa uso kupunguza adha ya mabomu ya machozi kama mmoja wapo anayeonekana kwenye picha hii.

hapa ndo maandamano yalipoanza kuvurigika na kila mtu kuchukua njia yake

Saturday, December 11, 2010

MASKINI ZITTO


Raymond Kaminyonge
KAMA ilivyotarajiwa na wengi, mbunge wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chadema, Zitto Kabwe amevuliwa wadhifa wake wa unaibu kiongozi wa upinzani bungeni, lakini chama hicho 'kikapigwa jeki' baada ya mfanyabiashara maarufu, Mustafa Sabodo kukipa Sh150 milioni kwa ajili ya kujenga chuo cha maadili ya uongozi.

Matukio hayo mawili pia yaliambatana na kuugua ghafla kwa Zitto na makamu mwenyekiti wa Chadema, Said Amur Arfi ambao wamelazwa Hospitali ya Aga Khan kwa matatizo tofauti.

Habari zilizopatikana jijini Dar es Salaam jana zinasema kuwa Zitto, ambaye pia ni naibu katibu mkuu wa Chadema, alipigiwa kura ya kutokuwa na imani naye na wabunge wa chama hicho kwenye mkutano wao uliofanyika juzi mjini Bagamoyo.
Hadi jana, hakuna kiongozi yeyote wa Chadema aliyepatikana kuzungumzia hatua hiyo, lakini wabunge waliohudhuria semina mjini Bagamoyo na ambao hawakutaka majina yao yatajwe, walisema kura hiyo ilipigwa baada ya kujadili kitendo chachake cha kupinga uamuzi wake wa wenzake kumsusia Rais Jakaya Kikwete wakati akitoa hotuba ya kuzindua Bunge la Kumi.

Pia wabunge hao walimtaka Zitto ajieleze kutokana na kitendo chake cha kupinga uamuzi wa pamoja wa kumsusia Rais Kikwete.
Uamuzi wa wabunge hao kumvua uongozi ulikuwa ukitarajiwa na wengi baada ya Zitto kupinga hadharani kitendo cha wenzake cha kutoka kwenye ukumbi wa Bunge wakati Rais Jakaya Kikwete akianza kuhutubia kuonyesha kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais na kushinikiza kuandikwa kwa katiba mpya na kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi.

Uamuzi wa kumsusia Kikwete ulifikiwa na wabunge hao baada ya mjadala mrefu ulioisha kwa kupiga kura. Zitto na wenzake tisa hawakuingia ndani ya ukumbi wa Bunge siku Kikwete alipokuwa akihutubia na baadaye kuitisha mkutano na waandishi wa habari kueleza kupinga kitendo cha wenzake.

Baada ya Zitto na wenzake kutoingia kwenye ukumbi wa Bunge ili watekeleze uamuzi wa kutoka nje wakati Rais Kikwete akianza kuhutubia, katibu mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa alisema waliosusia uamuzi hao wangechukuliwa hatua na kamati ya wabunge.

Baadaye mnadhimu wa kambi ya upinzani bungeni, Tundu Lissu alitangaza kumwandikia barua Zitto na wabunge wengine tisa ambao hawakuingia kwenye ukumbi wa Bunge siku ya uzinduzi, kuwataka wajieleze kwa kuwa walichofanya ni utovu wa nidhamu.
Wakati taarifa hizo za kuvuliwa uongozi wa Zitto zikibainika, mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini alilazwa tangu juzi saa 3:00 usiku kwenye Hospitali ya Aga Khan katika kipindi ambacho gazeti moja la kila siku limeripoti kuwepo kwa mpango wa kumuua.

Taarifa zinasema Zitto amelzwa wodi namba 57 iliyo ghorofa ya tatu na tayari amechukuliwa vipimo vyote ingawa madaktari wamesema hawakuona tatizo na kwamba wanasubiri kipimo kikubwa.
Akizungumza na gazeti hili akiwa hospitalini, Zitto aliwataka Watanzania kutokuwa na hofu na kuugua kwake kwa kuwa ni ugonjwa wa kawaida akiwataka wamuombee apone haraka.
"Watanzania wasiwe na wasiwasi na kuugua kwangu. Hii ni kawaida tu, madaktari wananipa matibabu niombeeni nipone haraka," alisema Zitto.

Alipoulizwa kuhusu mkutano huo, Zitto alisema hawezi kueleza lolote kwa kuwa alipata nafasi ya kuhudhuria siku moja kati ya mbili za mkutano huo.
Wabunge wengine wa Chadema, Lucy Owenya na John Shibuda walifika hospitalini hapo jana kumjulia hali Zitto ambaye alijijengea umaarufu katika Bunge la Tisa kutokana na uwezo wake wa kujenga hoja.
Zitto amekuwa akionekana kuwa na mwenendo tofauti na mwenyekiti wake Freeman Mbowe. Wakati wa uchaguzi mkuu wa chama hicho mwaka jana, Zitto alitangaza kugombea uenyekiti, uamuzi ambao ungempambanisha na Mbowe, lakini wazee wa chama hicho walimwita na kumshauri aondoe jina lake.

Chaguzi za umoja wa vijana wa chama hicho na baraza la wanawake pia ziliibua makundi yaliyoripotiwa kuwa ni ya wafuasi wa Zitto na Mbowe na chaguzi hizo zilivurugika na kuahirishwa.
Mara baada ya Chadema kuingiza wabunge wengi na hivyo kunyakua haki ya kuunda kambi ya upinzani, Zitto alitangaza kugombea uongozi wa kambi hiyo bungeni, lakini baadaye Mbowe alipewa nafasi hiyo.

Katika hatua nyingine, makamu mwenyekiti wa Chadema, Said Amur Arfi naye amelazwa wodi namba 29 iliyo ghorofa ya pili kwenye hospitali hiyo na habari ambazo hazijathibitishwa zinasema Arfi anasumbuliwa na matatizo ya kibofu cha mkojo.
Hata hivyo, jitihada za Mwananchi kutaka kuonana na kuzungumza na Arfi hazikufanikiwa jana.
Hata hivyo, Chadema ilipata ahueni baada ya Sabodo kuamua kuipa Sh150 milioni ili ifanikishe azma yake ya kujenga chuo cha maadili ya uongozi kitakachoitwa “Mustafa Sabodo Accademy” na mfanyabiashara huyo, ambaye ni kada wa CCM, akasema ataendelea kukisaidia kwa karibu zaidi chama hicho.

Msaada huo wa Sabodo kwa Chadema ni wa tatu katika kipindi kisichozidi miezi minne baada ya muumini huyo wa siasa za Mwalimu Julius Nyerere kukipatia jumla ya Sh200 milioni kabla na wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu.
Akitoa msaada huo jana kwa viongozi wa Chadema na wabunge, Sabodo alisema kuwa huo ni mwanzo na ataendelea kukisadia chama hicho kwa sababu kimeonyesha nia ya kuleta maendeleo nchini.

Alisema malengo ya elimu ni kufanya vitendo na sio kula pesa kama inavyofahamika kwa wengine, hivyo mchango wake wa elimu ameshautoa kwa chama fulani lakini hakuna maendeleo yoyote zaidi ya kupoteza pesa bure na badala yake yanabaki majengo tu badala.
“Hii si mara ya kwanza kutoa mchango kwa kuwa nimeshatoa kwa chama lakini hadi sasa hakuna kilichofanyika ila kwa hiki chama kimeonyesha kina malengo mazuri," alisema.

Alisema yeye ni Mtanzania na amezaliwa mkoa wa Lindi hivyo anaamua kuchangia chama chochote chenye kuonyesha lengo la kufanya maendeleo nchini na sio ubabaishaji na kwamba chama bora kinajulikana kwa vitendo si maongezi yasiyokuwa na msingi.
Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe alisema chuo hicho kitakuwa ni cha kwanza nchini chenye lengo la kuwapatia mafunzo viongozi wanaotaka kugombea nafasi mbalimbali ili wawe na uwezo wa kusaidia jamii.

“Tuna lengo la kuanzisha chuo cha kuwasaidia viongozi wawe bora na sio bora viongozi hivyo leo hii tunatangaza rasmi ujenzi wa chuo hicho na ndani ya miaka mitano utakuwa umeshakamilika," alisema Mbowe.
Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo Chadema itaendelea kumuenzi Sabodo kutokana na umuhimu wake katika chama hicho na taifa kwa ujumla, kama wanavyoenziwa viongozi wengine.

Alisema Sabodo huwa haogopi kama walivyo wafanyabiashara wengine ambao huwa wanaogopa kuchangia vyama vya upinzani kwa kuhofia usalama wao kutoka serikalini.

“Kipindi cha uchaguzi nilikuwa nawafuata wafanyabiashara ambao ni rafiki zangu, lakini walikuwa wanashindwa kunipa ushirikiano kwa kuniambia wazi kuwa wanaogopa vitisho vya serikali, lakini nilivyomfuata Mzee Sabodo aisaidie Chadema wakati wa uchaguzi, aliniambia niwaite waandishi wa habari ili umma ufahamu mchango wake kwa jamii,” alisema Mbowe.

Naye katibu mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa alisema leo kamati ya chama itakutana na kujadili gharama hizo na kuziweka wazi kwa vyombo vya habari, ikiwa ni changamoto kwa vyama vingine.

source: mwananchi gazeti

Tuesday, November 30, 2010

Wanafunzi wa Chuo cha Ustawi wa jamii wafanya Mgomoo!!


Wanafunzi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii jijini Dar es Salaam jana walifanya mgomo baridi wakidai mambo mbalimbali ikiwemo kubadilishwa uongozi wa chuo.

Madai mengine wanayodai ni pamoja na wanafunzi 400 kutofanyiwa udahili, huduma mbovu za vyoo na hostel zilizopo wanataka zitumike.

Mgomo huo ulianza jana saa 3:00 asubuhi ambapo wanafunzi walionekana katika makundi huki wengine wakiwa wanaimba nyimbo na wengine wakiwa wamebeba mabango yaliyoandikwa madai yao ikiwemo kutaka uongozi mpya wa chuo.

Hata hivyo, ilipofika majira ya saa 6:00 mchana, mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana, alifika chuoni hapo na alizungumza na uongozi wa chuo pamoja na serikali ya wanafunzi na kukubaliana kuwa Alhamisi watakwenda Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kukutana na Waziri wa Afya, kutafuta mwafaka.

Alisema kinachochangia kuwepo kwa matatizo chuoni hapo ni kutokuwepo kwa bodi na kusema kuwa ucheleweshaji wa kuundwa kwa bodi hiyo umetokana na kuingiliana na uchaguzi mkuu.

Alifafanua kuwa wanafunzi hao wana malalamiko ya msingi hivyo Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inatakiwa kuchukua hatua za haraka za kuunda bodi ili matatizo yaliyopo yaweze kushughulikiwa.

Rais wa wanafunzi wa chuo hicho, Gerald Simbeye, alisema wanaipa serikali wiki moja kuanzia jana ili kuona kama matatizo yao yataanza kushughulikiwa.

vipi wadau mnasemaje kuhusiana na hili, je ni kweli hatuwezi kupata maendeleo bila ya mapinduzi kama alivyosema katika moja ya theori za Carl Max!!!????

Tuesday, October 12, 2010

KURA YAKO MOJA INAWEZA KULETA MABADILIKO.

Ndugu watanzania zimebaki siku chache tuu kufikia tarehe 31 octoba 2010, ambapo wananchi wote wenye sifa ya kupiga kura watakuwa wakichagua viongozi wao ambao ni madiwani, wabunge na rais nchi nzima. Kila mwananchi aliyetimiza umri wa miaka 18 anahaki ya kupiga kura kufuatana na ibara ya 21 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Katika kipindi hiki nimekuwa nikifuatilia kampeni za wagombea na sera zao kutoka vyama mbalimbali, kusema kweli kuna tofauti kubwa na chaguzi za nyuma zilizotangulia. Kwa sasa watu wameonyesha mwamko mkubwa na mabadiliko ya kutaka kufuatilia kwa kina sera za wagombea na ilani za vyama vyao.

Ila kwa hali isiyo ya kawaida bado kuna wananchi wanaimani potofu kwamba hawatapiga kura kwa sababu kura yao moja haiwezi kubadilisha matokeo. Kwa kweli uamuzi huu unaofanywa na raia hauitaki mema nchi yetu ya Tanzania.Kuna msemo mmoja wa kiingereza unaosema ‘Try and fail than fail to try’ unamaana ni bora ujaribu na ushindwe kuliko ushindwe kujaribu.

Mimi ninapenda kusisitiza kwamba kura yako moja inaweza kuleta tofauti kubwa sana kwenye matokeo na pia tutambue kwamba tunapaswa kutumia nafasi yetu ya kikatiba kuchagua viongozi watakaotutumikia kwa kipindi kingine cha miaka mitano ijayo (2010 – 2015).

Ninaweza kukupa mfano dhahiri ambapo ulitokea kwenye moja ya uchaguzi mkuu wa rais katika nchi ya Marekani mwaka 1876. Uchaguzi huu ulihusisha wagombea wawili, mmoja kutoka chama cha Democratic ambaye alijulikana kwa jina la Samwel J. Tilden, na kutoka chama cha Republican aliyejulikana kama Rutherford B.Hayes.

Hayes alifanikiwa kushinda na kuwa rais wa Marekani kwa kumzidi mgombea mwenzake Tilden kwa kura moja tu. kwa hiyo unaweza kuona kwa jinsi gani kura moja inavyoweza kuleta mabadiliko, hasa katika nchi kama ya kwetu ambapo katiba inatambua mgombea kushinda kwa tofauti yoyote ya kura

Jamani wananchi wote wa Tanzania hasa vijana tujitokeze kwa wingi katika vituo vyetu vya kupigia kura siku jumapili ya tarehe 31 octoba 2010, ili tuweze kuchagua viongozi bora na si bora viongozi.
.

Monday, October 11, 2010

Thursday, September 30, 2010

JK APIGA KAMPENI KUFA NA KUPONA

Wakati wengine wakilalamika kwamba hawaoni kilichofanyika bado wapo ambao wanatambua nafasi ya Rais ambaye amemaliza muda wake wa miaka 5. Muheshimiwa Jakaya Kikwete. Hii ni kutokana na kugusa maisha yao mojamoja kama ilivyotokea kwa Dada yetu Bahati ambaye ni mlemavu.

JK akiongea na Bahati Iddi Nzimano, mwanadada mwenye ulemavu wa kutokuwa na mikono yote miwili ambaye mwaka juzi alimsaidia mtaji wa kufungua biashara na sasa Bahati maisha yake ni mswano kabisa licha ya ulemavu alionao.
JE, HUU NI USHABIKI WA KISIASA AU NI UHALISIA WA MAMBO, WE WASEMAJE???

RAIS MSTAAFU BEN MKAPA ALAMBA DUME KWA BAN KI-MOON


Mh. Mkapa aliteuliwa wiki iliyopita na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,Bw. Ban Ki-moon kuongoza timu ya watu watatu watakaofualitia na kuangalia kura ya maoni ya Sudan Kusini. Mh. Mkapa amesema kura hiyo ni ya muhimu sana kwa hatma ya mamilioni ya Wasudan ambao Januari tisa watapiga kura kuamua endapo eneo la Sudan Kusini lijitenge na kuwa taifa huru ama la na amesema la msingi ni kwa watu kukubali matokeo mara kura hiyo itakapokamilika.. Mh. Mkapa aliyazungumza hayo wakati wa mahojiano na mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya Redio ya Umoja wa Mataifa,B. Flora Nducha

Rais Mstaafu wa awamu ya tatu wa Tanzania,Mh. Benjamin W. Mkapa akiwa katika mahojiano na mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa,Bi Flora Nducha katika ofisi za Umoja wa Mataifa,jijini New York,Marekani.


Kwa kusikiliza mahojiano hayo ingia katika mtandao wa Redio ya Umoja wa Mtaifa http://www.unmultimedia.org/radio/kiswahili pia kwenye facebook http://www.facebook.com/UNRadioKis au waweza kubonyeza moja kwa moja kwenye mahojiano yenyewe http://www.unmultimedia.org/radio/kiswahili/detail/113198.html

Friday, August 6, 2010

JK ALIPOMTEMBELEA OBAMA WHITE HOUSE

JK akibadilishana mawazo na Rais wa marekani Barrack Obama ndani ya ikulu ya marekani.Waafrika wengi walikuwa na moyo uliojaa matumaini pale walipoona Rais Obama ambaye ni mmarekani mwenye asili ya Afrika huko Kenya ambako ni Afrika Mashariki. Ndoto hizi ambazo zimetimia kwa sasa zilitabiriwa na mpigania haki za mtu mweusi huko Marekani aliyeitwa Dk.Martin luther King jr. siku moja wakati akiwahutubia Wamarekani alisema" nina ndoto kuwa siku moja watoto wangu watatu watatambulika, sio kwa sababu ya rangi ya ngozi zao bali ni uwezo walio nao"

Haya yanatimia baada ya kumuona Rais Obama akiliongoza taifa lenye uwezo na nguvu za kivita kama Marekani. Sasa je, hapa Rais JK alipopata nafasi ya kukutana na Obama unafikiri watazungumza nini kwa mara ya kwanza?

DK. SLAA AENDELEA KUNGURUMA NCHINI KUTAFUTA WADHAMINI


Mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA Dk. Wilbroad Slaa akihutubia umati wa wakazi wa Mtwara alikoenda kutafuta udhamini

sehemu ya umati mkubwa wa wakazi wa Mtwara mkutanoni hapo


Mh. Mabere Marando akiongea wakati wa mkutano huo

Friday, July 9, 2010

4 Lessons from Billionaire College Entrepreneurs


There are more than enough college business success stories to go around - and I'm not talking about that dude who lived next to you in your dorm and made enough money for books by selling home-made Che Guevara t-shirts. I'm talking about the businesses that started in college and became billion-dollar companies. There's something to learn from the Zuckerbergs, Dells and Gateses of the world. Here are four of those lessons.
1. Find a Need and Fill It
This is the most basic of advice for starting a business; either find something that doesn't exist but would improve the lives of those around you, or find an already available product and make it better and cheaper. Mark Zuckerberg is probably the most famous and richest 26-year old on the planet right now, and he did exactly this when creating Facebook.
Zuckerberg was an undergrad at Harvard in 2004, taking computer science (go figure), and had been programming since he was in his teens. At Zuckerberg's old school there had been a registry of students and their photos published every year, but not at Harvard. So Zuckerberg set out to change that, but after his initial hacking into Harvard's server to retrieve the information needed to make a kind of "hot or not" Harvard page, he was shut down and had to go a different route. This gave rise to thefacebook.com and later, after he and his team moved to California,
There have certainly been problems and issues along the way, but what started as a desire to give everyone access to Harvard student photos has made Zuckerberg a billionaire. Facebook is expected to reach one billion accounts in the near future.
2. Think Outside of School
Michael Dell regularly ranks among the richest men in the world as the founder and CEO of Dell computers. Dell actually started this company while he was still in college doing his pre-med courses. Even as a teenager, Dell was interested in computers and finding out how electronics work, and while he was at college, he turned this into a part-time job. Dell started upgrading computers from a room in residence and eventually started operating as "PCs Limited" out of a condo, selling upgraded PCs via direct order. This eventually became Dell computers, which dominated the PC world during the 1990s and mid-2000s.
The company is not quite as dominant a PC force right now, but having started it as a hobby while pursuing an entirely different goal, Dell has certainly made his mark on the computer world.
3. Use Your School Projects for Larger Goals
When you're in college, it's best to try and focus your studies in a way that interests you and will work out in your favor once you're done school. So don't write a 2,000 word paper on Chapter 57 from "Moby Dick" unless you truly find it interesting or want to teach this Melville classic in the future; make your studies work for you.
This is what Larry Page and Sergey Brin did when they were both pursuing their PhDs at Stanford in computer science. They were working on a research project that would create a search engine that would analyze the relationship between websites, and Google was born. The idea of Google comes from Brin's and Page's idea that information should be accessible and universal, and they're making this a reality through a project started at Stanford.
4. Don't Let School Get in the Way
Bill Gates didn't let school get in the way of creating something that would both help the world and make him a multibillionaire. After scoring a mere 1590 out of 1600 on the SATs, Gates enrolled at Harvard with the hope of studying law, and after seeing one the first mass-consumed micro computers, the Altair 8800, Gates and his former classmate Paul Allen approached the maker of the computer to let them know they had written a programming language for the computer. After the maker of the computer, MITS, accepted the offer, Gates left Harvard to pursue his dream, never to return. Shortly after this, Microsoft was formed.
Gates used the college's computer labs to work towards his real passion, and when that passion paid off, he realized that college wasn't for him. Zuckerberg also left Harvard and hasn't returned.
The Bottom Line
There are many other success stories, like Frederick Smith who based the idea for FedEx on an economics paper he'd written while doing a bachelor's of economics at Yale, but the majority of money-making college entrepreneurs have been involved with computers. Overall, college entrepreneurs need to focus on their true passions and let schooling aid them in getting to this goal, and if schooling gets in the way, entrepreneurs have to be prepared to put it aside to follow their idea to the end.

Friday, June 18, 2010

VUVUZELA AND SOUTH AFRICA WORLD CUP 2010




lets go to south africa where the fifa world cup 2010 is taking place, here we gonna see some of the stadium and sound instrument which is called the vuvuzela. what is it?

What's plastic, a metre long, brightly coloured and sounds like an elephant? It's the vuvuzela, the noise-making trumpet of South African football fans, and it's come to symbolise the sport in the country.

It's an instrument, but not always a musical one. Describing the atmosphere in a stadium packed with thousands of fans blowing their vuvuzelas is difficult. Up close it's an elephant, sure, but en masse the sound is more like a massive swarm of very angry bees.

And when there's action near the goal mouth, those bees go really crazy.

To get that sound out requires lip flexibility and lung strength - in short, a fair amount of technique. So be sure to get in some practice before attending a South African football match, or you the sound you produce may cause some amusement in the seats around you!

Vuvuzela supplier Boogieblast offers this advice: "Put your lips inside the mouthpiece and almost make a 'farting' sound. Relax your cheeks and let your lips vibrate inside the mouthpiece. As soon as you get that trumpeting sound, blow harder until you reach a ridiculously loud 'boogying blast'.

hope u know it, visit again and again this blog.
south africa oyee, and africa oyee

DOLA INAZIDI KUWA JUU..

moja ya mitaa ya bongo katika bureau of exchange..

exchange rate inazidi kuwa juu nini tatizo???
kazi kwenu wadau maana wahenga wasema "fumbo ufumbie mjinga mwerevu ataling'amua"

HEY APPLY FOR ISWIT

The 2010 ISWiT will be hosted in Dodoma, Tanzania’s capital city and home to its House of Parliament, from the 8th to the 13th of August 2010 under the theme “THE VOICES OF YOUNG INTELLECTUALS ON CONSTRUCTING AFRICA ANEW; COME, LISTEN AND ACT…..!

The International Students Week in Tanzania (ISWITs) a thematic event where young people from Higher learning institutions across the globe get an opportunity create solutions, practice diplomacy, leadership and learn form the best in the field. They come together with an intention deliberating different global issues and come up with solutions and recommendations for dissemination to relevant organs for implementation. So far such an event organized only in Tanzania over all Higher learning institutions across Africa . Deliberations centre on diverse regional and global issues relevant to young people and development.

FOR REGISTERING GO TO WWW.ISWIT.ORG
DON'T MISS THIS..

Tuesday, June 1, 2010

NAKAAYA AJITOSA KUWANIA UBUNGE WA VITI MAALUMU ,MUZIKI APUMZIKA KIDOGO


Nakaaya Sumari akihurubia katika harakati zake za jamii


WAKATI vuguvugu la uchaguzi mkuu likiendelea kushika kasi nchini mwanamuziki wa maarufu wa kizazi kipya nchini,Nakaaya Sumari ameamua kujitosa katika kinyang”anyiro cha kuwania ubunge wa viti maalumu mkoani Arusha kupitia chama cha demokarisia na maendeleo(Chadema) kwa kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo mjini Arusha.

Nakaaya ambaye ni katibu mhamasishaji wa baraza la vijana wa Chadema wilayani Arusha alichukua fomu ya kuwania kiti hicho juzi katika ofisi za chama hicho zilizopo maneeo ya Esso jengo la Meru Plaza mjini Arusha.

Akiwa ameongozana na mwenyekiti wa vijana wa Chadema wilaya ya Arsuha.Exaud Mamuya sanjari na katibu wa vijana,Arnold Kamnde,mgombea huyo alichukua fomu ya kuwania kiti hicho majira ya saa 3;30 asubuhi katika ofisi hizo.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fomu ya kuwania kiti hicho Nakaaya alisema ya kuwa binafsi anahisi ya kuwa nafasi ya yeye kuwa mwakilishi wa wanawake wa mkoa wa Arusha katika bunge la jamhuri nchini kupitia chadema mkoani Arusha umewadia.

Nakaaya alisema ya kuwa lengo kubwa lililomsukuma kuwania nafasi hiyo ni kutokana na uchungu alionao hususani mateso wanayopata wakinamama katika masusla ya afya ya uzazi katika huku akihaidi kusimamia masula ya afya ya uzazi kwa wakianamama nchini.

“nahisi muda umefika wa kutenda ninayoyahubiri siku zote,nataka nikasimamie matatizo ya uzazi kwa wakinamama hili linanipa uchungu katika maisha yangu siku zote”

“nataka nikawawakilishe wnawake wa mkoa wa Arusha kupitia chama changu nina imani nitashinda nafasi hii kwasababu ninajiamini, hivyo naomba mniunge mkono wanawake’alisema Nakaaya

Awali akimkabidhi fomu ya kuwania nafsi hiyo katibu wa Chadema wilayani Arusha,Bakari Kasembe aliwataka wanawake wote wa mkoa wa Arusha kupitia chama hicho kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi hiyo.

Kasembe alisistiza ya kuwa awali chama chao hakikuwa na uwakilishi wa kiti hicho mkoani Arusha katika bunge la jamhuri nchini lakini wakati huu wamejipanga kutoa viti vitatu na kiti cha ubunge wa Arusha mjini.

Tayari joto la kuwania nafasi ya ubunge wa viti maalumu mkoani Arusha kupitia chama hicho limeanza kushika kasi ambapo hadi sasa tayari wagombea wawili wameshajitokeza kuwania kiti hicho ambao ni Magreth Olotu na Joyce Muya.

bonyeza hapa www.mtandaowawatanzania.blogspot.com

Zitto Kabwe


zitto njia panda..

NMB kutoa gawio la Shilingi 15 bilioni


Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ben Christiaanse (kushoto), akiongea na wanahisa wa benki hiyo kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa benki uliofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NMB, Misheck Ngatunga.

NA MWANDISHI WETU


WANAHISA wa Benki ya NMB watapata gawio la jumla ya Shilingi 15.7 bilioni kwa mwaka 2009, ikiwa ni ongezeko la asilimia 4.7 ikilinganishwa na mwaka uliotangulia.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NMB, Misheck Ngatunga, amesema mgawo wa kila hisa kwa mwaka utakuwa Shilingi 31.40, ikilinganishwa na Shilingi 30 kwa mwaka 2008.

Alikuwa anawasilisha ripoti ya mwaka 2009 kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa NMB uliofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Ngatunga alisema mwaka 2009 ulikuwa wa changamoto nyingi kutokana na kuongezeza kwa ushindani katika sekta za benki pamoja na mtikisiko wa uchumi duniani, ambao ulikuwa na madhara makubwa katika uchumi wa Tanzania kama kwingineko duniani.

Aliisifu serikali kwa kuandaa mkakati wa kukabiliana na mtikisiko wa uchumi kwa kuendeleza mfuko wa kuokoa na kusaidia sekta na taasisi zilizoathirika na mtikisiko huo.


“Sekta ya fedha ya Tanzania kwa ujumla haikuathirika na mtikisiko huo, na iliendelea kuwa na mtaji wa kutosha na yenye faida. Ingawa athari hizo zilikuwa tofauti kwa kila benki.”Hata hivyo, alisema hali ya uchumi na kushuka kwa viwango vya riba vilichangia kushuka kidogo kwa mapato na faida mwaka 2009, ambapo benki hiyo ilipata faida ya Shilingi 68.04 bilioni (kabla ya kodi), ikilinganishwa na Shilingi 70.94 bilioni mwaka uliotangulia.


Upungufu huo wa faida ni kwa asilimia nne.Wakati huo huo, NMB imedhamiria kuboresha huduma zake na kupunguza msongamo wa wateja katika matawi yake nchini na kuwafikia Watanzania wengi zaidi wanaoshi vijijini.

Katika taarifa yake ya mwaka 2009, benki hiyo yenye mtandao mkubwa nchini imesisitiza kuwa itazingatia zaidi kupunguza muda wa wateja kusubiri katika matawi na ATM, pamoja na kuboresha mikopo.

Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi alisema pamoja na mafanikio mengi yaliyopatikana katika kipindi kipindi cha mwaka uliopita, ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa matawi na mtandao wa ATM kutoka 167 mwaka 2008 hadi 281 mwishoni mwa mwaka 2009, bado wanakabiliwa na changa moto nyingi, ikiwemo tatizo la msongamano wa wateja.

“Nina uhakika kwamba uongozi na wafanyakazi wa NMB watafanikiwa kukabiliana na changamoto hizo,” alisema Ngatunga.Alisema NMB inakusudia kupanua zaidi mtandao wa matawi nchini ili kuweza kujikita zaidi katika msukumo wa ‘Kilimo Kwanza’, mpango wa kuboresha uzalishaji wa kilimo na sekta ya mabadiliko kwa nia ya mapinduzi ya kilimo.

Akizungumza katika mkutano huo, Mtendaji Mkuu wa NMB, Bern Christiaanse, alisema mtandao wa matawi ya NMB uliongezeka kufikia 133 mwaka 2009, huku matawi mapya nane yakifunguliwa mwaka huo.

Alisema ongezeko hilo ni matokeo ya mkakati wa benki hiyo wa kutoa huduma za kifedha kwa watanzania wengi iwezekanavyo.Kwa mujibu wa taarifa ya mwaka 2009, jumla ya raslimali za benki hiyo zilikua kwa asilimia 20.6 kutoka Shilingi 1,384.3 bilioni hadi 1,669.3 bilioni, wakati ambapo mtaji wa benki ulikua kwa asilimia 20.4 kutoka Shilingi 159,689 milioni hadi Shilingi 192,239 milioni.

Taarifa hiyo iliyowasilishwa kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa NMB ni ya pili tangu benki hiyo iwe kampuni ya umma baada ya kuorodheshwa kwenye soka la hisa la Dar es Salaam.

kwa habari zaidi tembelea: www.issamichuzi.blogspot.com

Monday, May 31, 2010

LAUNCHING OF UDOM MARKETING SOCIETY TAKES PLACE AT DODOMA HOTEL



marketing students from udom

Prof Casmir M. Rubagumya listen the speaker at the high table

Principal of college of social science Prof Casmir M. Rubagumya declared the opening of the market society of Udom officially

its time to eat the food at the dodoma hotel....

waohhhh the food was so delicious!!!!!!




the hall event was sponsored by Zain mobile phone company and the students who taking marketing at the university of Dodoma

Thursday, May 27, 2010

NEWS NEWS :TRAINING OF ENTREPRENEUSHIP IN DODOMA

Tanzania Youth Vision Association[TYVA] is a youth led organization with non-profit, non-partisan, non governmental "NGO" founded in 2000 and registered in 2002 to work in civil society having key focusing on youth awareness raising and empowerment.

Vision: To see a free, just, democratic and peaceful society, in which there is active and effective youth participation. check more www.tyvatz.or.tz

TANZANIA YOUTH VISION ASSOCIATION (TYVA - DODOMA) has prepared the training program of entrepreneurship which will be facilatated by the facilitator from the SIDO. This is for all member and anyone who is interested to join and participate in this program. The program will be held next week on 3rd up to 5th of May 2010. so for more information you may contact with: MANASE KAVISHE - TREASURER- TYVA DODOMA ( MOB NO. 0714 204027, UDOM)

VERY POISONOUS AND DANGEROUS CREATURES


The Brazilian Wandering Spider (Phoneutria) or banana spider appears in the Guinness Book of World Records 2007 for the most venomous spider and is the spider responsible for most human deaths.
This spider is believed to have the most potent neurotoxic venom of any living spider. Only 0.006mg (0.00000021oz) is sufficient to kill a mouse. They are also so dangerous because of their wandering nature. They often hide during daytime in highly populated areas inside houses, clothes, boots, and cars.
Its venomous bite causes not only intense pain, the venom of the spider can also cause priapism - uncomfortable erections lasting for many hours that lead to impotence.


If you ever happen to be running through the rain forests somewhere in Central or South America, do not ever pick up beautiful and colorful frogs - it can be the Poison Dart Frog. This frog is probably the most poisonous animal on earth.The 2 inch long (5cm) golden poison dart frog has enough venom to kill 10 adult humans or 20,000 mice. Only 2 micrograms of this lethal toxin (the amount that fits on the head of a pin) is capable of killing a human or other large mammal. They are called dart frogs because indigenous Amerindians use of their toxic secretions to poison the tips of their blow-darts.. Poison dart frogs keep their poison in their skins and will sicken or kill anybody who touches or eats it.

Jelly box can be found in the waters around Asia and Australia

The prize for The Worlds Most Venomous Snake goes to the Inland Taipan of Australia. Just a single bite from this snake contains enough venom to kill 100 human adults or an army of 250,000 mice. Its venom is at least 200 - 400 times more toxic than a common cobra. The Inland Taiwans extremely neurotoxic venom can kill an adult human in as little as 45 minutes. Fortunately this snake is very shy and there have been no documented human fatalities (all known bites were treated with antivenin).



The King Cobra (Ophiophagus hannah) is the worlds longest venomous snake - growing up to 5.6 m (18.5 ft) in length. Ophiophagus, literally means snake-eater as it eats other snakes.. One single bite of this deadly snake can easily kill a human. This snake is even capable of killing a full-grown Asian Elephant within 3 hours if the larger animal is bitten in a vulnerable area such as the trunk.
Its venom is not as toxic as other venomous snakes, but King Cobra is capable of injecting 5 times more venom than black mamba and can result in mortality up to 5 times faster than that of the black mamba. It is quite widespread, ranging across South and South-east Asia, living in dense highland forests.

Tuesday, May 25, 2010

OBAMA NAYE TICHA...


Lazima utaelewa tu....

thats hw people are..........

DAVID SEAMAN NDANI YA KILIMANJARO

David Seaman aliyekuwa mlinda mlango wa timu ya uingereza miaka michache atembelea mlima Kilimanjaro uliopo nchini Tanzania.

Tony Pulis akitoa zawadi ya kikombe kwa nahodha wa timu ya Zara Tours, John. Zara Tours ndio mabingwa wa mashindano ya kampuni za utalii mkoa wa Kilimanjaro

David Seamen akiwa na waongoza watalii wa kampuni ya Zara Adventure mlima Kilimanjaro walikopanda Mei 19 kwa lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya kituo cha watoto cha Donna luis Hospice ch a nchi Uingereza.

David Seamen akionyesha ishara ya ushindi mara baada ya kurejea salama kutoka mlima Kilimanjaro alikopanda na wenzake 13.