KARIBUNI SA

Friday, June 18, 2010

VUVUZELA AND SOUTH AFRICA WORLD CUP 2010




lets go to south africa where the fifa world cup 2010 is taking place, here we gonna see some of the stadium and sound instrument which is called the vuvuzela. what is it?

What's plastic, a metre long, brightly coloured and sounds like an elephant? It's the vuvuzela, the noise-making trumpet of South African football fans, and it's come to symbolise the sport in the country.

It's an instrument, but not always a musical one. Describing the atmosphere in a stadium packed with thousands of fans blowing their vuvuzelas is difficult. Up close it's an elephant, sure, but en masse the sound is more like a massive swarm of very angry bees.

And when there's action near the goal mouth, those bees go really crazy.

To get that sound out requires lip flexibility and lung strength - in short, a fair amount of technique. So be sure to get in some practice before attending a South African football match, or you the sound you produce may cause some amusement in the seats around you!

Vuvuzela supplier Boogieblast offers this advice: "Put your lips inside the mouthpiece and almost make a 'farting' sound. Relax your cheeks and let your lips vibrate inside the mouthpiece. As soon as you get that trumpeting sound, blow harder until you reach a ridiculously loud 'boogying blast'.

hope u know it, visit again and again this blog.
south africa oyee, and africa oyee

DOLA INAZIDI KUWA JUU..

moja ya mitaa ya bongo katika bureau of exchange..

exchange rate inazidi kuwa juu nini tatizo???
kazi kwenu wadau maana wahenga wasema "fumbo ufumbie mjinga mwerevu ataling'amua"

HEY APPLY FOR ISWIT

The 2010 ISWiT will be hosted in Dodoma, Tanzania’s capital city and home to its House of Parliament, from the 8th to the 13th of August 2010 under the theme “THE VOICES OF YOUNG INTELLECTUALS ON CONSTRUCTING AFRICA ANEW; COME, LISTEN AND ACT…..!

The International Students Week in Tanzania (ISWITs) a thematic event where young people from Higher learning institutions across the globe get an opportunity create solutions, practice diplomacy, leadership and learn form the best in the field. They come together with an intention deliberating different global issues and come up with solutions and recommendations for dissemination to relevant organs for implementation. So far such an event organized only in Tanzania over all Higher learning institutions across Africa . Deliberations centre on diverse regional and global issues relevant to young people and development.

FOR REGISTERING GO TO WWW.ISWIT.ORG
DON'T MISS THIS..

Tuesday, June 1, 2010

NAKAAYA AJITOSA KUWANIA UBUNGE WA VITI MAALUMU ,MUZIKI APUMZIKA KIDOGO


Nakaaya Sumari akihurubia katika harakati zake za jamii


WAKATI vuguvugu la uchaguzi mkuu likiendelea kushika kasi nchini mwanamuziki wa maarufu wa kizazi kipya nchini,Nakaaya Sumari ameamua kujitosa katika kinyang”anyiro cha kuwania ubunge wa viti maalumu mkoani Arusha kupitia chama cha demokarisia na maendeleo(Chadema) kwa kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo mjini Arusha.

Nakaaya ambaye ni katibu mhamasishaji wa baraza la vijana wa Chadema wilayani Arusha alichukua fomu ya kuwania kiti hicho juzi katika ofisi za chama hicho zilizopo maneeo ya Esso jengo la Meru Plaza mjini Arusha.

Akiwa ameongozana na mwenyekiti wa vijana wa Chadema wilaya ya Arsuha.Exaud Mamuya sanjari na katibu wa vijana,Arnold Kamnde,mgombea huyo alichukua fomu ya kuwania kiti hicho majira ya saa 3;30 asubuhi katika ofisi hizo.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fomu ya kuwania kiti hicho Nakaaya alisema ya kuwa binafsi anahisi ya kuwa nafasi ya yeye kuwa mwakilishi wa wanawake wa mkoa wa Arusha katika bunge la jamhuri nchini kupitia chadema mkoani Arusha umewadia.

Nakaaya alisema ya kuwa lengo kubwa lililomsukuma kuwania nafasi hiyo ni kutokana na uchungu alionao hususani mateso wanayopata wakinamama katika masusla ya afya ya uzazi katika huku akihaidi kusimamia masula ya afya ya uzazi kwa wakianamama nchini.

“nahisi muda umefika wa kutenda ninayoyahubiri siku zote,nataka nikasimamie matatizo ya uzazi kwa wakinamama hili linanipa uchungu katika maisha yangu siku zote”

“nataka nikawawakilishe wnawake wa mkoa wa Arusha kupitia chama changu nina imani nitashinda nafasi hii kwasababu ninajiamini, hivyo naomba mniunge mkono wanawake’alisema Nakaaya

Awali akimkabidhi fomu ya kuwania nafsi hiyo katibu wa Chadema wilayani Arusha,Bakari Kasembe aliwataka wanawake wote wa mkoa wa Arusha kupitia chama hicho kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi hiyo.

Kasembe alisistiza ya kuwa awali chama chao hakikuwa na uwakilishi wa kiti hicho mkoani Arusha katika bunge la jamhuri nchini lakini wakati huu wamejipanga kutoa viti vitatu na kiti cha ubunge wa Arusha mjini.

Tayari joto la kuwania nafasi ya ubunge wa viti maalumu mkoani Arusha kupitia chama hicho limeanza kushika kasi ambapo hadi sasa tayari wagombea wawili wameshajitokeza kuwania kiti hicho ambao ni Magreth Olotu na Joyce Muya.

bonyeza hapa www.mtandaowawatanzania.blogspot.com

Zitto Kabwe


zitto njia panda..

NMB kutoa gawio la Shilingi 15 bilioni


Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ben Christiaanse (kushoto), akiongea na wanahisa wa benki hiyo kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa benki uliofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NMB, Misheck Ngatunga.

NA MWANDISHI WETU


WANAHISA wa Benki ya NMB watapata gawio la jumla ya Shilingi 15.7 bilioni kwa mwaka 2009, ikiwa ni ongezeko la asilimia 4.7 ikilinganishwa na mwaka uliotangulia.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NMB, Misheck Ngatunga, amesema mgawo wa kila hisa kwa mwaka utakuwa Shilingi 31.40, ikilinganishwa na Shilingi 30 kwa mwaka 2008.

Alikuwa anawasilisha ripoti ya mwaka 2009 kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa NMB uliofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Ngatunga alisema mwaka 2009 ulikuwa wa changamoto nyingi kutokana na kuongezeza kwa ushindani katika sekta za benki pamoja na mtikisiko wa uchumi duniani, ambao ulikuwa na madhara makubwa katika uchumi wa Tanzania kama kwingineko duniani.

Aliisifu serikali kwa kuandaa mkakati wa kukabiliana na mtikisiko wa uchumi kwa kuendeleza mfuko wa kuokoa na kusaidia sekta na taasisi zilizoathirika na mtikisiko huo.


“Sekta ya fedha ya Tanzania kwa ujumla haikuathirika na mtikisiko huo, na iliendelea kuwa na mtaji wa kutosha na yenye faida. Ingawa athari hizo zilikuwa tofauti kwa kila benki.”Hata hivyo, alisema hali ya uchumi na kushuka kwa viwango vya riba vilichangia kushuka kidogo kwa mapato na faida mwaka 2009, ambapo benki hiyo ilipata faida ya Shilingi 68.04 bilioni (kabla ya kodi), ikilinganishwa na Shilingi 70.94 bilioni mwaka uliotangulia.


Upungufu huo wa faida ni kwa asilimia nne.Wakati huo huo, NMB imedhamiria kuboresha huduma zake na kupunguza msongamo wa wateja katika matawi yake nchini na kuwafikia Watanzania wengi zaidi wanaoshi vijijini.

Katika taarifa yake ya mwaka 2009, benki hiyo yenye mtandao mkubwa nchini imesisitiza kuwa itazingatia zaidi kupunguza muda wa wateja kusubiri katika matawi na ATM, pamoja na kuboresha mikopo.

Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi alisema pamoja na mafanikio mengi yaliyopatikana katika kipindi kipindi cha mwaka uliopita, ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa matawi na mtandao wa ATM kutoka 167 mwaka 2008 hadi 281 mwishoni mwa mwaka 2009, bado wanakabiliwa na changa moto nyingi, ikiwemo tatizo la msongamano wa wateja.

“Nina uhakika kwamba uongozi na wafanyakazi wa NMB watafanikiwa kukabiliana na changamoto hizo,” alisema Ngatunga.Alisema NMB inakusudia kupanua zaidi mtandao wa matawi nchini ili kuweza kujikita zaidi katika msukumo wa ‘Kilimo Kwanza’, mpango wa kuboresha uzalishaji wa kilimo na sekta ya mabadiliko kwa nia ya mapinduzi ya kilimo.

Akizungumza katika mkutano huo, Mtendaji Mkuu wa NMB, Bern Christiaanse, alisema mtandao wa matawi ya NMB uliongezeka kufikia 133 mwaka 2009, huku matawi mapya nane yakifunguliwa mwaka huo.

Alisema ongezeko hilo ni matokeo ya mkakati wa benki hiyo wa kutoa huduma za kifedha kwa watanzania wengi iwezekanavyo.Kwa mujibu wa taarifa ya mwaka 2009, jumla ya raslimali za benki hiyo zilikua kwa asilimia 20.6 kutoka Shilingi 1,384.3 bilioni hadi 1,669.3 bilioni, wakati ambapo mtaji wa benki ulikua kwa asilimia 20.4 kutoka Shilingi 159,689 milioni hadi Shilingi 192,239 milioni.

Taarifa hiyo iliyowasilishwa kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa NMB ni ya pili tangu benki hiyo iwe kampuni ya umma baada ya kuorodheshwa kwenye soka la hisa la Dar es Salaam.

kwa habari zaidi tembelea: www.issamichuzi.blogspot.com