KARIBUNI SA

Monday, November 28, 2011

Posho za wabunge zapanda kimyakimya:ZAPANDA KUTOKA SH70,000 HADI 200,000, NI ZAIDI YA ASILIMIA 150

Wabunge wakiwa katika moja ya vikao vya bunge mjini Dodoma
HUKU mjadala wa kufutwa au kwa posho za wabunge na watumishi wengine wa Serikali ukiwa umefifia, posho za vikao (sitting allowance) za wabunge zimepanda kutoka Sh70,000 kwa siku hadi Sh200,000, imefahamika.

“Zimeongezeka kutoka Sh70,000 mpaka 200,000, wameanza kulipwa Bunge lililopita hili ni ongezeko la karibu mara tatu, yaani asilimia 154,” kilieleza chanzo chetu kutoka ndani ya Ofisi za Bunge.

Kutoka na ongezeko hilo, kwa sasa kila mbunge atakuwa akilipwa Sh80,000 ikiwa ni posho ya kujikimu (perdiem) anapokuwa nje jimbo lake, posho ya vikao (sitting allowance) Sh200,000 na mafuta ya gari Sh50,000 kila siku, ambazo jumla yake ni Sh330,000 kwa siku.

Kutokana na ongezeko hilo, Bajeti ya Bunge kwa ajili ya posho za vikao vya wabunge imepanda na kufikia Sh28 bilioni kwa mwaka.

Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alipoulizwa kuhusu taarifa hizo alisema hawezi kuzungumzia jambo hilo kwa sababu siyo msemaji wa wabunge, bali Ofisi ya Bunge.

“Ni nani kawapa hizo taarifa bwana, au ni vyanzo vyenu vya habari?” alihoji Dk Kashililah.

Baada ya kuelezwa kuwa taarifa hizo zimetoka kwenye vyanzo vyetu vya kuaminika alisema “Hao wana utaratibu wao bwana, labda mtafute Spika ndiye msemaji wa Wabunge.”

Juhudi za kumpata Spika, Anne Makinda kutoa ufafanuzi wa suala hili, hazikufanikiwa baada ya simu yake kuita wakati wote bila kupokewa hata pale alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu (sms) hakujibu. Hata simu zote za Naibu wake, Job Ndugai hazikupatikana.

Hata hivyo, Mbunge wa Ludewa (CCM), Deo Filikunjombe alisema kuongezeka kwa posho hizo kunatokana na wabunge kuwa wanalipwa mishahara midogo kulingana na kazi wanayofanya.

Alisema endapo wawakilishi hao wa wananchi wangekuwa wanalipwa mishahara inayolingana na kazi wanayofanya, kusingekuwa na sababu ya kuongezeka kwa posho hizo.

“Ninachosema mimi, siyo wabunge peke yao, lakini watumishi wote wa umma wanalipwa mishahara midogo sana mimi binafsi sitegemei posho za Bunge, kabla ya kuingia bungeni nilikuwa nimefanya kazi kwa miaka 14 na nilikuwa napata mshahara mzuri tu,” alisema Filikunjombe.

Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa alisema amezisikia taarifa hizo za kuongezeka kwa posho lakini siyo kwa undani. Hata hivyo alisema hakuwa katika nafasi nzuri ya kuzungumza suala hilo.

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alisema walivyokuwa wakipinga posho hizo wakati zilivyokuwa Sh70,000 waandishi wa habari walichukua suala hilo kama ajenda ya Chadema, hivyo kupandishwa kwa posho hizo ni matokeo ya watu kuwapuuza walivyokuwa wakizipinga.

“Msimamo wetu sisi tulishautoa tangu wakati posho zikiwa Sh70,000 wakati sisi tukipinga hizi posho waandishi wa habari na Watanzania mlichukulia suala hili kama ajenda ya Chadema, sisi wenyewe tupo wachache bungeni, tulichotaka ni kuonyesha jinsi fedha za Watanzania zinavyotumika vibaya,” alisema na kuongeza:

“Achilia mbali hizo 200,000 za wabunge kuna watu huko serikalini wanalipwa mpaka Sh400,000 au Sh1 milioni kwa siku nyie ulizeni.”

Alipoulizwa kama amechukua posho hiyo ya Sh200,000 alisema hajafanya hivyo kwa sababu hazifuatilii.

“Sijui hata kama zimeanza kulipwa au la kwa sababu huwa sizifuatilii na haka kama suala la posho hilo zilijadiliwa wakati wa vikao vya mwanzo mimi sikuwepo kwa sababu tulikuwa kwenye kesi yetu Arusha na bungeni tulikuja mwishoni wakati wa Muswada wa Katiba,” alisema Mbowe.

Ongezeko hili la posho za wabunge limekuja wakati Watanzania wakiendelea kuishi kwenye maisha magumu yanayochangiwa na mfumuko wa bei ambao mpaka mwisho mwa Oktoba ulikuwa umefikia asilimia 17.9.

Pia ongezeko hili limekuja wakati Watanzania wakiwa na matumaini ya posho hizi kupunguzwa baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kutangaza bungeni kuwa Serikali imekubali pendekezo la kutafakari na kuziangalia upya posho mbalimbali wanazolipwa wabunge na watumishi wote umma.

Mbunge wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali alisema kuwa hawezi kuzungumza chochote juu ya posho hizo kwa kuwa hajapata barua rasmi juu ya kupanda kwake.

“Sijapata barua yoyote, nikiuliza na kupata majibu kwa wahusika nitakuwa na uhakika na nitakupa maoni yangu na msimamo wangu vizuri kabisa, lakini kwa sasa siwezi kusema chochote,” alisema Mkosamali.

Juni 7, mwaka huu Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Zitto Kabwe, aliwasilisha barua Ofisi ya Bunge akikataa posho akisema watumishi wa Serikali na wabunge, hawastahili kulipwa posho wanapohudhuria vikao rasmi vya uwajibikaji wao wa kawaida.

Zitto alisema posho hiyo haistahili kulipwa kwake, wabunge wengine wala watumishi wa umma kwa kuwa kuhudhuria vikao ni sehemu ya kazi zao.

Alisema kitendo cha Waziri Mkuu kueleza kuwa watatafakari na kuangalia upya na kwamba suala la posho ni sera ya taifa na Ilani ya Uchaguzi ya CCM, ni ishara ya kiongozi huyo wa juu kukubali wazo la Chadema na safari ya kufuta posho hizo.

Awali, mara baada ya Chadema kutangaza msimamo huo, Spika Makinda alipinga uamuzi wa kususia posho akisema suala hilo lipo kisheria na kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kuamua kuliondoa.

Alisema wabunge wa Chadema wataendelea kulipwa posho za vikao kupitia akaunti zao za benki na watatakiwa kusaini fomu ya mahudhurio ya Bunge, vinginevyo watajiweka katika wakati mbaya.

Hata hivyo, akihitimisha hoja za wabunge katika hotuba yake ya makadirio ya matumizi ya ofisi yake na zilizo chini yake juzi, Pinda alisema suala la posho lipo kwenye mchakato wa kuangaliwa upya.

Thursday, November 10, 2011

How to Forgive yourself

No matter what the occasion, we often find ourselves looking for the best gift possible to give those we care about.  We want to find some token of our affection to give them that says, “I care about you.”  Of course, the best gifts to give those around us aren’t those that can be bought in any store.  To show how much we love others, we need to let go of the hurt and pain that they have caused and forgive them.  Love and forgiveness along with second chances are the best gifts we can possibly give to others.

 But what about yourself?  Have you thought about giving yourself the gift of forgiveness this year?  Are you ready to be free and ready to move ahead into a life of graciousness and love in the future?  If you are, you must forgive yourself for the mistakes you’ve made – and that can be a difficult thing to do!  It’s easy to try and hide our mistakes and not think about them, but what we hide has power over us; 
it can sit there in the back of our minds and fester, eating away at our self-assurance and our sense of God’s love for us, making us wonder if we are truly worthy.  We have to let go of our mistakes and forgive ourselves just as God forgives us.  And He does forgive us, completely and with no reservations!

“You are a God ready to forgive, gracious and merciful.”
- Nehemiah 9:17

“Do not judge, and you will not be judged; do not condemn, and you will not be condemned.  Forgive, and you will be forgiven.”
- Luke 6:37

When you are ready to forgive yourself, there are six steps that I’ve found very helpful in helping me on the path to self-forgiveness.  Perhaps they will help you in your struggle to let go of you past mistakes and embrace forgiveness:

Six Steps Toward Forgiving Yourself

1.   Take out a sheet of paper and write your name at the top.  Now take some time to think about all of those things you’ve never let go of in your past that you haven’t forgiven yourself for.

2.   Write down what those transgressions are and who you hurt; how you hurt them, etc.  Was it verbal or physical abuse?  Dishonesty? Neglecting someone you cared about? Betrayal? Rejection? Theft? Rape? Lying? Addiction? Adultery?

3.   Write down how you feel about yourself because of these unresolved feelings over your past mistakes.  Be very honest with yourself.  Although you may have made amends or been forgiven by others, do you still feel unworthy?  God knows how you feel and He sees your heart.  Express on paper how you feel and let the emotions flow – release them!

4.   Decide to forgive yourself.  Forgiveness is not a feeling but a decision of the will and one of the greatest Gifts from God.  He has told us to forgive and that He will give us the power to do so – but it all begins with the decision to do so.

5.   Take your list to God and acknowledge your forgiveness to Him.  “Lord, I come to You today and give up my unforgiveness.  I forgive myself for ____________________.  At this moment, I choose not to hold these offenses against myself, but put them into Your Hands.  God, heal my emotional wounds and help me to be able to move forward without regrets and help me to let go of the past and start fresh.  God give me the ability to  offer upliftment and comfort to someone else with the same comfort you have given me.   I release my past sins of ____________into Your Hands.”

6.   Destroy the list in private.  This visual exercise can be very freeing.  Whether you decide to shred it, burn it  or tear it up and scatter it in the trash, imagine your past mistakes being destroyed and floating away in the same manner.
This is what it means to be “born again.”  The Lord doesn’t want us to dwell on what has happened before – our lives as Christians are about who we are now and in the future, walking in forgiveness and love.  So give yourself a wonderful gift that is free of charge and yet priceless this year – forgive yourself!

Prayer:
Heavenly Father,
Alone with You in this moment of meditation and prayer, I release any unresolved feelings of resentment or regret.
Help me through this process of healing.
I release to you any unresolved feelings that I have toward myself.  I understand that not forgiving myself is disobedience toward you.
Forgive me for any pain that I have caused in the lives of others.  Forgive me for not letting go of the past and moving forward in love.
I experience now the relief of forgiveness to the depths of my being.
Heavenly Father, I acknowledge and give thanks for Your love that strengthens me, comforts and soothes me emotionally, mentally, physically and spiritually.
In the complete fullness of Your Love, I can and do forgive myself.
Thank you, Heavenly Father, for healing my heart and bringing Joy and Meaning back into my life.
In the Name of Jesus, Amen.
Source: Hosanna Inc.