KARIBUNI SA

Tuesday, March 23, 2010

WANACHUO IFM WAGOMA


Madenti wa chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) jana waligoma kuingia darasani. Mgomo uliosababisha na kile ambacho madenti hao walichokilalamikia kupanda kwa ada pasipo mpangilio na taarifa yoyote. madenti hao ambao wengi wao wanasoma katika chuo hicho kwa ufadhili wa bodi ya mikopo ya elimu ya juu (HESLB) wanalalamika kuwa bodi haiwezi kuongeza ada kwa kiasi kilichoongezeka. madenti hao wamedai kuwa hawaitambui serikali ya wanafunzi katika chuo hicho kwa sababu haijatoa tamko lolote hadi wao walipofikia hatua ya kugoma. pia wanachodai mpaka sasa ni matokeo yao ambayo hawajayapata. Jamani sisi watoto wa maskini tuliopo vyuoni kwa nini tunanyanyaswa hivi, mhusika fikiri na kisha chukua hatua?

No comments:

Post a Comment